Mkuu
wa wilaya ya kibondo Bw Venance Mwamoto (kushoto) akiangalia dodoso
zilizochanwa na makarani wa sensa ya watu na makazi (picha na James Jovin )
|
Watu
wawili makarani wa sensa wilayani Kibondo mkoani Kigoma wanashikiliwa na jeshi
la polisi wakituhumiwa kuchana dodoso za sensa ya watu na makazi inayoendelea kwa
sasa nchini.
Jeshi
la polisi limesema kuwa makarani hao ni pamoja na Elisha Claudias ambaye ni mwanafunzi wa chuo
kikuu dodoma pamoja na Fredrick Mhalafu mkazi wa Kibondo mjini.
Mkuu
wa wilaya ya kibondo Bw Venance Mwamoto ambaye pia aliongozana na mkuu wa jeshi
la polisi Bw Marko Joshua amewataka makarani kuendelea na zoezi la sensa na
kuwahakikishia kuwa watalipwa posho yao yote.
Mkuu wa wilaya ya kibondo Venance Mwamoto
akimpa mama mwenye watoto mapacha aliyekuwa amekataa kuhesabiwa zawadi ya
shilingi elfu 10 ya kukubali kkuhesabiwa na makarani wa sensa
|
Jeshi
la polisi wilayani Kibondo limesema kuwa
Elisha alichana dodoso alizokuwa ameshika Fredrick katika kituo walichopangiwa cha
Kifura shule ya msingi katika tarafa ya Kifura kata ya Busunzu wilayani kibondo.
Aidha
tukio hilo lililotokea Jumatatu August 26 huko kifura wakati vijana hao pamoja
na makarani wenzao wakijaribu kushinikiza kulipwa posho zao baada ya kuletewa
posho nusu kinyume na makubaliano yao.
Mkazi
wa kifura Kibondo Issa Jumma akiwa kwenye gari la polisi tayari kwa kupelekwa
mahabusu baada ya kugoma kata kata kuhesabiwa katika zoezi la sensa ya watu na
makazi.
|
Makarani
hao wa sensa ya watu na makazi wanashikiliwa na jeshi la polisi wilayani Kibondo
kwa uchunguzi zaidi wa tukio hilo ambapo pia limewataka makarani kuendelea na
zoezi la sensa na kutochana madodoso kwa kuwa ni kosa kisheria .
Mama
huyo anatoka katika familia ya bw issa juma mkazi wa busunzu kibondo ambapo
yeye pamoja na kaya nyingine tatu waligoma kuhesabiwa kutokana na maadili ya
dini zao (picha na James Jovin).
|
Chanzo:jamesjovin.blogspot.com
No comments:
Post a Comment